19 Juni 2026 - 10:17
Qalibaf: Tutatekeleza Maelekezo ya Kiongozi wa Mapinduzi na Kulinda Haki za Taifa la Iran

Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema ujumbe wa Kiongozi wa Mapinduzi ni ramani ya njia ya kurejesha haki za taifa la Iran na Kambi ya Muqawama, akisisitiza kuwa hawataruhusu upande mwingine kukiuka ahadi wala kukanyaga haki za wananchi wa Iran.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (AS) –ABNA-, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amepongeza ujumbe wa hekima na msukumo uliotolewa na Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, akisema utakuwa mwongozo mkuu katika hatua za Iran za baadaye.

Katika taarifa yake aliyomuelekeza Kiongozi wa Mapinduzi, Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei, Qalibaf alisema kuwa maelekezo hayo yameweka wazi kuwa kutiwa saini kwa waraka wa makubaliano si mwisho wa safari, bali ni mwanzo wa hatua ngumu za kurejesha haki za wananchi wa Iran na Kambi ya Muqawama kutoka kwa adui anayekiuka ahadi zake.

Aidha, alisisitiza kuwa Bunge la Iran litayafanya maelekezo ya Kiongozi wa Mapinduzi kuwa dira yake, na halitaruhusu upande mwingine kutumia ukiukaji wa makubaliano au vitisho kuhujumu haki za taifa la Iran na Kambi ya Muqawama. Pia alieleza kuwa ujumbe huo umeimarisha uwezo wa Iran wa kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa ahadi na wajibu wa Marekani chini ya makubaliano hayo.

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha